Mke Amuokoa Mume Aliyetaka Kujiua Toka Ghorofani kwa Kushikilia Boxer

Mwanamke Huyu Ilibidi Amshikilie Jamaa kwa Dakika 20 Mpaka Waokoaji Walipofika
Mwanaume mmoja aliyetaka kujiua ilibidi aokolewe mara baada ya kujirusha toka ghorofani na mkewe kuwahi kuikamata boxer yake.

Mashahidi wanasema Ling Su alining'inia kwa muda wa dakika 20 kabla ya mapolisi na waokoaji kufika.
 
Alikuwa ananing'inia toka kwenye ghorofa ya sita maeneo ya Changchun, jimbo la Jilin, mashariki ya China.
 
Mlango kwenye nyumba hiyo ulikuwa umefungwa, kitendo kilichozuia shughuli ya uokowaji huo kuwa wa haraka.
 
'Tulisikia sauti na kelele na kulikuwa na mtu akinaning'inia dirishani huku mke wake akiwa ameishikilia boxer yake,' alisema mpita njia mmoja.

'Hakika alikuwa na nguvu za kutosha kuweza kumshikilia huku akiwa anapiga kelele kutaka msaada.
 
'Tulikuwa tunataka kutoa msaada ila nyumba ilikuwa imefungwa na tulishindwa kuuvunja mlango' waliongezea kwa kusema.

Majirani walichungulia kupitia madirishani mwao ili kuona kwa ukaribu tukio hilo.

Waokowaji walifanikiwa kumvuta na kumuokoa jamaa huyo mwenye umri wa miaka 45 aitwaye Wang Li, ambaye anasemekana kuwa na msongo wa mawazo kutokana na kutokuwa na kazi.


Waokoaji Walifanikiwa Kumuokoa Jamaa Huyu Mwenye Msongo wa Mawazo ya Kutokuwa na Kazi
 (DailyMail)

No comments:

Post a Comment