Msanii Keko Wa Uganda Amekuwa Chizi?Keko

Keko

Mitandao mingi ya kijamii imeejaa habari za rapa wa kike kutoka Uganda zikisema kwa amekuwa chizi, na hiini baada ya kuonekana akimkimbiza kibaka wa laptop.
Mitandao hiyo ya kijamii pia imeeleza kwamba Star huyo aliandika kwenye ukurasa wake wa twitter jinsi gani Uganda imekuwa si sehemu salama kwake na kuna watu wanahatarisha maisha yake, watu ambao walitaka kufahamu zaidi kuhusu stori hiyo, walijaribu kumpigia simu lakini matokeo yake ilipokelewa na dereva wa boda boda na hata alichokiongea kilionekana kutokuleta maaa yoyote.
Kitendo hicho cha Keko, kimewalazimu baadhi ya watu kuhitimisha kuwa amechizika, habari za hivi karibuni zinadai kuwa uchizi wa stori ya Keko ulikuwa ni stunt tu, aliyoitumia kufanya utafiti kujua ni kiasi gani anajulikana na watu
Keko ambae sasa yuko chini ya Sony Music Entertainment ameahirisha uzinduzi wa album yake mara tatu sasa ambapo alitangaza kuizindua mwezi wa nne tarehe 17 mpaka mwezi wa tano tarehe 4 na sasa kuipeleka mpaka mwezi wa nane tarehe 10, na inasemekana Sony nao wanataraji kutangaza siku yao ya kuzindua album hiyo.
read more "Msanii Keko Wa Uganda Amekuwa Chizi?Keko"

Man to Watch

Mbwana Samatta
Ilikuwa ni dakika ya 44 krosi toka kwa Trésor Mputu inatua kichwani kwa MBWANA SAMATTA na kuandika bao la pili, full time Zamalek 1 v TP Mazembe 2
Nyota wa Tanzania, Mbwana Ally Samata, jana alipiga Bao la pili na la ushindi kwa Timu yake TP Mazembe iliyoifunga Al Zamalek bao 2-1 katika Mechi ya klabu bingwa barani Afrika iliyochezwa huko Cairo, Misri bila ya Watazamaji wowote kufuatia kuzuiwa kwao kuingia kwenye Mechi baada ya Vifo Uwanjani kutokana vurugu mapema Mwaka huu.
TP Mazembe ya Congo DR ilitangulia kupata bao katika Dakika ya 34 lililofungwa na Hichani Homoonde na Al Zamalek wakasawazisha Dakika moja baadae kwa bao la Razak Omotoyossi.
Al Ahly ya Misri walitoka sare bao 1-1 huko Ghana na Bechem Chelsea lakini bado wanaongoza Kundi B wakiwa na Pointi 10 wakifuatiwa na TP Mazembe.
Katika michuano ya kombe la shirikisho, timu iliyoitoa Simba ya Tanzania  Al Ahli Shandi kutoka Sudan ilipata ushindi ugenini wa bao 1 – 0 dhidi ya GD Interclube ya Angola.
 
read more "Man to Watch"

Top 10 Music Video za Kinigeria Zinazoongoza kutazamwa zaidi kwenye Youtube

P-Square
1. P-Square - Do
 Me 8,190,758 views

2. P-Square ft. Akon & May D - Chop My Money
 7,858,903 views

3. D'Banj - Oliver Twist
 5,035,658 views

4. Flavour - Nwa Baby (Ashawo Remix) Video
 4,457,160 views

5. P-Square - Beautiful Onyinye ft. Rick Ross [Official Video]
 3, 729, 635 views

6. P Square Ft J. Martins E No Easy (Official Video)
 2,912,350 views

7. Flavour - Oyi Remix ft. Tiwa Savage [Video]
 2,231,915 views

8. 5.Bracket - Girl Ft. Wizkid 3,208,276 views

9. VConnect Fever Video 2,018,238 views

10. P-Square - Forever
 1,906,905 views
read more "Top 10 Music Video za Kinigeria Zinazoongoza kutazamwa zaidi kwenye Youtube"