Mke wa Rais wa Ufaransa Akimbizwa Hospitali Baada ya Kubaini Mahusiano ya Mume Wake na Kimada

Mke wa Rais wa Ufaransa Valerie Trierweiler mapema mnamo siku ya Ijumaa ilibidi akimbizwe hospitali mara baada ya kupata habari kwamba mume wake ambaye ni Rais wa Ufaransa, Francois Hollande, kuhusishwa kuwa na mahusiano na mwanamke mwengine wa nje.
Ofisi yake imesema Mwanamke huyo alikimbizwa hospitali kwa ajili ya mapumziko na kufanyiwa vipimo.

Mwanamke huyo ambaye yupo kwenye mahusiano na Mr Hollande bila ya ndoa alikimbizwa hospitali mara baada ya jarida la Closer kuchapisha picha zilizoonyesha mahusiano yake ya nje.

Kiongozi huyo wa Ufaransa hajakataa kwamba alifanya ziara ya siri kumtembelea muigizaji wa kike aitwaye Julie Gayet kwenye gorofa karibu na Elysee Palace ila amehoji kwa nini aingiliwe uhuru wa maisha yake binafsi.

No comments:

Post a Comment