Jennifer Lopez Ahusishwa Skendo ya Picha za Utupu

Umeandika Mtandao wa Sohh:

Kwa mujibu wa taarifa, jamaa anayeitwa Rodrigo Ruiz amefungua kesi dhidi ya J. Lo akidai kwamba mwanamuziki na muigizaji huyo alimuomba yeye amtumie picha zake za utupu pamoja na demo ya mziki wake.

Anasema barua hiyo ilimpelekea kuamini kwamba ana nafasi kwenye maisha yake ya kimuziki na hata kwenye mahusiano ya kimapenzi na Lopez, ila  sababu J.Lo hakuendelea kufatilia hivyo jamaa alikuja kukata tamaa.

Ruiz amesema amekwazika sana maana alitegemea angekuja kuwa mtu mkubwa. Ruiz alitutumia machache ya kwenye barua yenye mistari mitatu ambayo aliipokea toka kwa “Lopez” ila ukiyasoma utaona kama ni ujinga … 

Ya kwanza ilisoma, “Nataka nikufahamishe kwamba nakukumbuka na bado nipo na nia nawe. Nina mpango wa kuachana na mume wangu. Ila siwezi kusema zaidi kwa muda huu hivyo tuishie hapa kwa sasa. Nitumie picha zako zote ukiwa na nguo na bila kuwa na nguo.”

(Mtandao wa TMZ umeandika)

Kwa bahati mbaya, kumbe kuna mwanamke mwengine mwenye umri miaka 53 ambaye ndiye anaweza kuwa nyuma ya mkasa huu.
 

Kwa kuongeza juu ya shitaka hilo, Ruiz amefungua kesi ya polisi akidai kunyanyasika kijinsia. Ruiz bado anaamini Lopez alituma barua zile kwake, ila kumbukumbu zinaonyesha Sanduku la Posta (S.L.P) alilotumia linamilikiwa na mwanamke anayeishi L.A mwenye umri wa miaka 53. 

Tulimpigia kumuuliza shitaka na kila kitu kingine, na kwa uwoga alijieleza kuwa yeye anahusika kwenye kushughulikia mabadilishano ya barua za washabiki wa Jennifer Lopez… Kisha akatukatia simu.

Muwakilishi wa wa J.Lo aliieleza TMZ, “hili ni suala dogo linaloonekana lina nia ya kuchafua jina lake, Ms Lopez hajawahi kumuona wa kukutana na mshitaki, pia hajawahi kuwasiliana naye. Tunaamini jambo hili kwani linatakiwa kupuuzwa na kufutwa.”

(TMZ Imeandika)

No comments:

Post a Comment